Saturday, October 27, 2012

AHADI YA MUNGU HUTUJENGEA IMANI ITUPAYO HAKI.


Ahadi za Mungu.
   Mungu amefanya ahadi nyingi kwa mwanadamu; ahadi za uponyaji, mafanikio, heshima, hekima, ufaulu katika masomo na nyingine nyingi. Na wengi wetu tunazifahamu vizuri ahadi hizo alizotuahidi Mungu; tunazisoma katika neno lake takatifu, Biblia na pia tunazisikia kupitia watumishi mbalimbali wa Mungu.
Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya, Kwa maana wewe upo pamoja nami”,  na  Zaburi 119:50 “Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imeniuhisha”.
   Kupita kati ya bonde la uvuli wa mauti (Zaburi 23:4) na kuwa katika taabu (Zaburi 119:50) ni kuingia au kupitia katika hali zenye changamoto mbalimbali za kiafya; magonjwa na udhaifu wa mwili, kielimu; kushindwa kutimiza malengo yako, kiuchumi; hali ngumu ya kiuchumi au kukosa ajila licha ya kuwa na elimu stahiki, kijamii; kukosa watoto kwa miaka mingi katika ndoa na hata jamii inakuita tasa, kufiwa na watoto pale tu wanapozaliwa na changamoto za namna nyingine nyingi. Katika neno la Mungu hapo juu tunafundishwa kwamba kuna nyakati tutaingia katika changamoto, taabu au bonde la uvuli wa mauti katika maisha yetu. Jambo la kujiuliza hapa, je tuingiapo katika changamoto au taabu hizo tunachukua hatua gani? Je, tumekuwa ni watu wa kumlaumu Mungu kwanini ameruhusu tuingie katika taabu? Na kama tumekuwa ni watu wa kulaumu na tunasubiri majibu kutoka kwa Mungu hakika Mungu hata tujibu kamwe, kwa sababu Mungu hana majibu ya lawama. Mungu anayo majibu ya maneno au maombi yenye hoja zilizojengwa katika imani ya neno lake tu.
   Na ndiyo maana kupitia mistari ya neno la Mungu hapo juu anatufundisha kuwa na imani kwa ahadi zake kwetu.  Anaposema “sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami”, Mungu kuwa pamoja naye ni kwamba ahadi ya Mungu ya ukombozi imemfunika na ni lazima atatoka katika bonde hilo la uvuli wa mauti, na “ahadi yako imeniuhisha” anamaanisha hawezi kukata tama pasipo kujali anapitia taabu ya namna gani kwa sababu ukombozi wake unakuja tena uko karibu.
   Na sisi tunapopitia katika mahangaiko, taabu, shida na misukosuko ya maisha tusiwe ni watu wa kulaumu na kulalamika mbele za Mungu, bali tuwe ni watu wenye kusimama katika maombi yenye imani ya ukombozi tukiziangalia ahadi za Mungu katika taabu zetu.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts