Monday, April 1, 2013

ISIPOKUWA MLIAMINI BURE.

1 WAKORINTHO 15:1-2

BASI NDUGU ZANGU NAWAARIFU ILE INJILI NILIYOWAARIFU, AMBAYO NDIYO MLIYOIPOKEA, NA KATIKA HIYO MNASIMAMA, NA KWA HIYO MNAOKOLEWA: IKIWA MNAYASHIKA SANA MANENO NILIYOWAHUBIRI; ISIPOKUWA MLIAMINI BURE.

Neno la Mungu (hapo juu) linatuambia habari ya injili ambayo kwa hiyo tunapokea zawadi au neema ya kuokolewa na kupokea uzima wa milele. Injili ya YESU KRISTO ambayo ndani yake kuna nguvu ya kutuokoa.

Ili upokee wokovu ni lazima uisikie injili ya Yesu Kristo na habari ya Ufalme wa Mungu Baba, pasipo injili ya Yesu Kristo hakuna wokovu, injili ya Yesu Kristo pekee!

Matendo ya mitume 10:3-6.

Kornelio, mtu mtauwa (hajaokoka bado) anatokewa na malaika katika maono, anaambiwa atume mtu kwa Simoni Petro, aje nyumbani mwake amwambie yampasayo kutenda….

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts