Monday, September 12, 2016

SADAKA

Bwana Yesu asifiwe mpendwa msomaji wetu!

Tunajiandaa kwenda kuwatembelea wazee na walemavu wa ukoma waishio katika nyumba za wazee hapa jijini Mwanza, serikali imefanya sehemu yake ya kuwajengea nyumba za kuishi, na sisi kama kanisa la Mungu kwa umoja wetu tunadhamiria kufanya kwa sehemu yetu kadiri Mungu atakavyotubariki. Tunategemea kuwapelekea mahitaji muhimu kwa maisha kama vile; chakula na mavazi.

Tunajipa muda wa mwezi mmoja tangu sasa (12/09/2016), ifikapo tarehe 12/10/2016 tunatarajia kuwa tumejipanga na kujiandaa vya kutosha.

Tunapenda ushiriki baraka hizi pamoja nasi, vile unavyobarikiwa na jumbe mbali mbali ndani ya "blog" hii, SILAGO2.BLOG na namna unavyomshuhudia Mungu kukutana nawe katika maisha yako na hata kufunguliwa kwa namna moja ama nyingine, tunapenda umshangilie Mungu kwa furaha iliyoambata na sadaka yako ili kuwasaidia wenye uhitaji.

Mungu anasema ikiwa twajisifu tuna dini iliyo safi (dini sahihi), na hatuwatazami wahitaji katika dhiki yao, twajidanganya. Dini iliyo safi ni kuwatazama (kuwasaidia) wahitaji (yatima, wajane, wazee) katika dhiki yao (Yakobo 1:27)

Na utoapo sadaka yako, toa kwa moyo wa kupenda (Zaburi 54:6), pia hakikisha unaisemea jambo sadaka yako kuhusu maisha yako ya kiroho au kimwili kulingana na uhitaji wako (Zaburi 50:5).

Ili kushiriki baraka hizi, unaweza kutuma mchango wako wa fedha kwa M-pesa kupitia namba;
0759 982 604 au kwa kutoa sadaka yako ya mali (siyo fedha) wasiliana nasi HAPA.

Tunakaribisha watu wote pasipo kujali tofauti za imani/dini zetu.

Mungu abarikiye, na atakwenda kukubariki kwa kadiri ya utakavyo toa na imani yako. Amina.

Sunday, September 11, 2016

MWANZO MPYA WA MILELE NDANI YA YESU KRISTO

Ufunuo wa Yohana 21:5
...tazama, nayafanya yote kuwa mapya...

Bwana Yesu asifiwe!
Ninakusalimu kupitia Jina la Yesu Kristo mpendwa msomaji wangu.

Kuna swali napenda ujiulize mpendwa msomaji wangu, leo nakwenda kuongea na mtu mmoja au nafsi moja, naongea na wewe!
SWALI; Licha ya neema, baraka, ulinzi na mema yote Mungu anayokutendea katika maisha yako (Yeremia 29:11-12), kwanini unatenda au unadhamiria kutenda dhambi???
Inawezekana wewe siyo mtu sahihi kwa swali hili, lakini yupo mtu sahihi ambaye ujumbe huu utakwenda kumponya na kumfanya kiumbe kipya. Kama wewe ni mtu sahihi kwa swali hili, je umewahi kujiuliza swali hilo hapo juu??? Viongozi wa dini na hata waumini wenzako wanadhani unaendelea vema, kumbe uliisha jitenga na imani kitambo sana, na yupo mpendwa mwingine anajulika kuwa anatenda dhambi na wapendwa wakimkanya anajifanya kuomba ushahidi, nikuulize swali, umewahi kwenda mbele za Mungu na kumwambia akupe ushahidi wa uovu wako? Najua huwezi kufanya hivyo kwa sababu Mungu hadhihakiwi na hadanganywi na jambo!

Kwa maana hiyo, hauwadanganyi viongozi wako wa dini na wapendwa, haujifichi mbele zao, hauwezi pia kumdanganya au kujificha mbele za Mungu, BALI unaidanganya nafsi yako. Kwanini kujidanganya nafsi basi???

JIBU; ...mungu wa dunia hii (ibilisi/shetani) amepofusha fikira zao, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo...(2 Kor 4:4)
Hakuna mwanadamu atendaye dhambi kwa matakwa yake binafsi, isipokuwa ametiwa upofu nafsini na ndani ya nia yake na ibilisi asione aibu ya dhambi. Kutenda dhambi ni aibu, tena nasema ni aibu, kama ilivyo kwa timamu kutembea bila nguo. Na hii ndiyo sababu dhambi hutendwa kwa kificho, gizani kwani anayepofusha na kumfanya mwanadamu atende dhambi ni mfalme wa giza, shetani au ibilisi. Na mtenda dhambi hutenda dhambi kwa kutimiza matakwa ya ibilisi/shetani...yaani, shetani hutumia mwili wa mwanadamu kutenda dhambi au kufanya uovu; kufanya uzinzi, uasherati, uuaji, wizi, tamaa mbaya iletayo mauti n.k (Waefeso 2:1-2)

Mpenzi msomaji wangu, sihukumu nafsi ya mtu kwa maana sipo katika nafasi ya kuhukumu, mwenye kuhukumu na kurehemu/kusamehe dhambi ni Mungu peke yake kupitia Kristo Yesu. Leo Mungu amekuona, kupitia damu ya Yesu Kristo atakwenda kukusamehe na kukutakasa kabisa.

Wednesday, August 31, 2016

SALAMU KATIKA KRISTO YESU, BWANA WETU

Bwana Yesu asifiwe, mpendwa msomaji wetu!
Tunakusalimu kupitia Jina la Yesu Kristo, Jina liponyalo na liokoalo. Amina.

Tunapenda kuwajulisha wasomaji wetu wote kuwa, baada ya kimya cha miaka takribani miwili sasa tunarudi tena hewani kwa nguvu mpya katika Jina la Yesu Kristo. Tegemea kubarikiwa, kukutana na Mungu na hata kupokea uponyaji kwani Yesu Kristo tumuaminiye hashindwi na jambo ikiwa imani yetu haiteteleki.

Jiandae na somo lenye kichwa, "MWANZO MPYA WA MILELE NDANI YA YESU KRISTO". Ni somo litakalokwenda kuimalisha maisha yako ya kiroho na kuinua imani yako zaidi kwa utukufu wa Mungu mwenyewe. Usikose!!!

Mungu wa mbinguni aishiye milele, akubariki sana. Amina.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts