Monday, September 12, 2016

SADAKA

Bwana Yesu asifiwe mpendwa msomaji wetu!

Tunajiandaa kwenda kuwatembelea wazee na walemavu wa ukoma waishio katika nyumba za wazee hapa jijini Mwanza, serikali imefanya sehemu yake ya kuwajengea nyumba za kuishi, na sisi kama kanisa la Mungu kwa umoja wetu tunadhamiria kufanya kwa sehemu yetu kadiri Mungu atakavyotubariki. Tunategemea kuwapelekea mahitaji muhimu kwa maisha kama vile; chakula na mavazi.

Tunajipa muda wa mwezi mmoja tangu sasa (12/09/2016), ifikapo tarehe 12/10/2016 tunatarajia kuwa tumejipanga na kujiandaa vya kutosha.

Tunapenda ushiriki baraka hizi pamoja nasi, vile unavyobarikiwa na jumbe mbali mbali ndani ya "blog" hii, SILAGO2.BLOG na namna unavyomshuhudia Mungu kukutana nawe katika maisha yako na hata kufunguliwa kwa namna moja ama nyingine, tunapenda umshangilie Mungu kwa furaha iliyoambata na sadaka yako ili kuwasaidia wenye uhitaji.

Mungu anasema ikiwa twajisifu tuna dini iliyo safi (dini sahihi), na hatuwatazami wahitaji katika dhiki yao, twajidanganya. Dini iliyo safi ni kuwatazama (kuwasaidia) wahitaji (yatima, wajane, wazee) katika dhiki yao (Yakobo 1:27)

Na utoapo sadaka yako, toa kwa moyo wa kupenda (Zaburi 54:6), pia hakikisha unaisemea jambo sadaka yako kuhusu maisha yako ya kiroho au kimwili kulingana na uhitaji wako (Zaburi 50:5).

Ili kushiriki baraka hizi, unaweza kutuma mchango wako wa fedha kwa M-pesa kupitia namba;
0759 982 604 au kwa kutoa sadaka yako ya mali (siyo fedha) wasiliana nasi HAPA.

Tunakaribisha watu wote pasipo kujali tofauti za imani/dini zetu.

Mungu abarikiye, na atakwenda kukubariki kwa kadiri ya utakavyo toa na imani yako. Amina.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts