Tuesday, February 20, 2018

MPANGO KAZI WA KIBIBLIA WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAISHA

Nakusalimu mpenzi msomaji wangu, Jina la Yesu Kristo lisifiwe.

Leo napenda kuanza na hadithi kwa ufupi sana,
Ninaishi katika jamii ya wafugaji ambao hutegemea malisho ya mifugo yao; ng’ombe, mbuzi na kondoo katika majani yaotayo kondeni na vichakani. Wengi wa wafugaji hawa wanamiliki idadi kubwa ya mifugo, hivyo huwalazimu kutoka na mifugo yao kila siku kwenda kutafuta malisho na maji. Vijana wa kiume wa umri wa kati, huamka mapema asubuhi, hutoa mifugo katika mazizi yao, huiswaga na kuiongoza mifugo hii sehemu yalipo malisho mazuri na maji. Kila ifikapo jioni, hufanya kama walivyofanya asubuhi, huiswaga na kuiongoza mifugo yao kuirudisha mazizini mwao. Wafugaji hawa wanaotembea na mifugo yao kwa lengo la kutafuta malisho na maji huitwa wachungaji.

Wachungaji hawa hukaa nyuma na kuitanguliza mifugo yao mbele kwa lengo la kuweza kuiangalia isitawanyike na kufanya uharibifu wa mazao na mazingira wawapo njiani kuelekea malishoni ama kurudi mazizini. Katika kundi la mifugo isiyopungua hamsini, mifugo iliyotangulia mbele huchoka kutokana na safari ya mwendo mrefu kwenda na kurudi kutafuta malisho, hivyo hupunguza mwendo kasi wa kutembea. Mifugo iliyotangulia mbele ikipunguza mwende kasi wa kutembea, huilazimu mifugo yote inayofuata pamoja na mchungaji kupunguza mwendo kasi. Mara tu mwendo kasi wa kutembea unapopungua mchungaji huichapa mifugo iliyo karibu naye, mifugo ya nyuma, ili iweze kuongeza mwendo pasipo kujali kuwa mifugo iliyo mbele ndiyo inayopunguza mwendo hivyo basi mifugo ya mbele ndiyo ilistahili kuchapwa. 

Mifugo ya nyuma iliyochapwa huanza kukimbia na kuisukuma mifugo ya mbele, ambayo hukumbuka, kumbe tumepunguza mwendo, na kuanza kukimbia pia ili kuongeza mwendo. Mifugo ya mbele inajisahau kutunza mwendo kasi, inaanza kutembea taratibu, ili kukumbushwa kuongeza mwendo kasi, inachapwa mifugo ya nyuma ambayo siyo sababu ya kupungua kwa mwendo kasi. Mara baada ya kuchapwa, huikumbusha mifugo ya mbele kuongeza mwendo kasi, na mara mwendo kasi unaongezeka. Hayo ndiyo maisha ya kila siku ya mifugo inayobaki nyuma katika msafara wa kwenda ama kurudi malishoni. Hupokea kipigo kisicho na sababu. 

Tujifunze nini katika hadithi ya leo? Hadithi ya leo inatufundisha mambo makubwa matatu; 1. Changamoto ni lazima 2. Usilalamikie changamoto 3. Kabiliana na changamoto. 

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts