Bwana Yesu asifiwe, mpendwa msomaji wetu!
Tunakusalimu kupitia Jina la Yesu Kristo, Jina liponyalo na liokoalo. Amina.
Tunapenda kuwajulisha wasomaji wetu wote kuwa, baada ya kimya cha miaka takribani miwili sasa tunarudi tena hewani kwa nguvu mpya katika Jina la Yesu Kristo. Tegemea kubarikiwa, kukutana na Mungu na hata kupokea uponyaji kwani Yesu Kristo tumuaminiye hashindwi na jambo ikiwa imani yetu haiteteleki.
Jiandae na somo lenye kichwa, "MWANZO MPYA WA MILELE NDANI YA YESU KRISTO". Ni somo litakalokwenda kuimalisha maisha yako ya kiroho na kuinua imani yako zaidi kwa utukufu wa Mungu mwenyewe. Usikose!!!
Mungu wa mbinguni aishiye milele, akubariki sana. Amina.