KISWAHILI

UNADHANI WEWE NI NANI?


Maana ya swali “unadhani wewe nani?”
Unadhani wewe nani ni aina ya swali linalokusudiwa kumkejeli ama kumdharau anayeulizwa likiambatana na kumnyooshea au kutomnyooshea kidole. Swali hili huelekezwa kwa anayekejeliwa ama dharauliwa kwa minajili ya kumshusha kiuwezo wa ufanisi wa jambo. Mara nyingi watu wanaoogopa uwezo wa mtu mwingine mfano katika mashindano hututmia swali hili ili kudhoofisha upande pinzani. Watu wasiojitambua uwezo wao mara nyingi hubabaishwa na swali hili.


Unadhani wewe nani? Swali hudhamiria kumchanganya anayeulizwa na kujiona hafai au hana thamani mbele za muulizaji. Kwa mfano, unaweza kumueleza mtu Fulani malengo yako makubwa unayotegemea kuyatimiza na hata ukamuomba msaada wa kimawazo ili kukupa nguvu zaidi ya kutimiza ndoto zako hizo. Badala ya kukuwezesha kimawazo na mtazamo mtu huyo anakuuliza, “unadhani wewe nani?” utimize mambo makubwa haya, wengi wamejaribu wameshindwa itakuwa wewe? Ama mtu anaamua kukukatisha tu tamaa kwa sababu anaamini utakapofanikiwa utafanyika kikwazo katika biashara zake. Kwa hiyo njia pekee ya kujiepusha na changamoto ya ushindani huo ni kukuwekea vikwazo vya kutofanikiwa ikiwamo kukufanya ujione hauwezi, haustahili na huna thamani ya kufanikiwa.

Kwanini watu huchagua kuwa wakatisha tamaa na kuvunja moyo?
Wakatisha tamaa huchagua kuwa hivyo kwa manufaa yao binafsi, kwa sababu wanatamani wao peke yao ndio wapate mema tu siku zote wakati wengine wakitaabika. Wakatisha tamaa huamaini wanapowasaidia wengine kuinuka na kufanikiwa itawafanya wao kushika na kufilisika, ndiyo sababu hawachagua kumsaidia ama kumtia moyo mtu yoyote ili afanikiwe. Huona raha kuwaona wengine wakifeli na kutaabika. 

Wakatisha tamaa ni sawa na wachawi. Mara nyingine huamua kumshusha aliyeko juu ama kumfilisi aliyekwisha fanikiwa. Watu wanapofeli, wanapoanguka na kushindwa kusonga mbele katika mambo mbali mbali, hiyo ndiyo furaha ya wakatisha tamaa. 

Kupambana na wakatisha tamaa
Huna haja ya kupambana na mkatisha tamaa yoyote katika maisha yako, wameamua kuishi na kuwa hivyo. Unapokatishwa tamaa usione kama kikwazo cha kukufanya usonge mbele, ona kama fursa ya kukupa uwezo wa kufanya makubwa zaidi ya hata uliyoyakusudia kwanza. Mtu anapokukatisha tamaa siyo kwa sababu nyingine isipokuwa ameona mafanikio na kung’ara zaidi katika maisha yako. Unapoamua kupambana na wakatisha tamaa wako, unapoteza muda wako na muelekeo wako kimaisha. Waache wapambane kushindana nawe na kamwe hawatashinda.
Usipoteze muda kushindana na mwanadamu anayekukatisha tamaa. Muoneshe uwezo wako kwa vitendo katika kufanikisha yale anayokukatisha tamaa na ikiwezekana fanikisha na ziada.

Hakuna nguvu itakayosimama kinyume nawe ikashinda
Hakuna nguvu itakayoshindana nawe ikashinda endapo utajitambua na kuujua uwezo ulioumbiwa. Wewe ni kiumbe wa ajabu na pekee uliyeumbiwa uwezo wa kufanikisha jambo lolote pasipo kumtegemea mwanadamu endapo tu utasimama imara katika kumtegemea Mungu. Mungu amekuumba kwa mfano wake. Kuyatambua haya haitoshi kukupa nguvu za kusimama na kusonga mbele katika ya vikwazo wa wakatisha tamaa? Kama haitoshi, soma mstari ufuatao, “Tuseme nini basi? Mungu akiwa upande wetu nani aliyekinyume chetu akashinda?” tafsiri kutoka Biblia takatifu, Warumi 8:31. Hakuna mwanadamu, hakuna maneno yoyote ya kulaani, hakuna nguvu zozote zinazoweza kusimama mbele yako na kukushinda endapo Mungu atakuwa upande wako. Jiamini katika uwezo Mungu alikuumba nao na umuamini Mungu, hakika hakuna litakaloweza kukuzuia kufanikisha jambo lolote linalompendeza na kumpa utukufu Mungu.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts