Friday, April 27, 2018

IMARISHA MAHUSIANO YAKO YA NDOA NA MAHUSIANO YAKO NA MUNGU


Mpendwa msomaji, ninakusalimu kupitia Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.

Nina habari njema kwako zenye baraka kutoka kwa Mungu. Neno la Mungu linatuagiza waamini kutomuacha elimu aende zake. Nini basi makusudi ya agizo hilo? Hakuna muamini anayeweza kukua na kuimarisha uelewa na ufahamu wake kwa habari ya elimu ya dunia na elimu ya Mungu pasipo kuwa na mpango madhubuti wa kuitafuta na kuikamata elimu hiyo. 

Huwezi kumtumikia Mungu ipasavyo kama hauna elimu ya kutosha kumuhusu. Na kama haumtumikii Mungu inavyostahili, hauwezi kukua kiroho kwa viwango vya utakatifu vinavyohitajika. Vivyo hivyo, hauwezi kuandaa ndoa yenye upendo imara (wanaotarajia kufunga ndoa) au kuwa na ndoa imara iliyojaa upendo, kujali na kuthamini kama hautakuwa na elimu kuhusu ndoa kwa mujibu wa Biblia takatifu. Hauwezi kuimarisha mahusiano yako ya ndoa au mahusiano yako na Mungu kupitia maombi peke yake, ni lazima usome. 

Habari njema ninazokuletea leo ni tarajia vitabu vizuri vyenye uwepo wa Mungu na uvuvio wa nguvu za Roho Mtakatifu kwa Jina la Yesu Kristo.

Kitabu cha kwanza kinaitwa, “THE HAPPIEST EVERLASTING MARRIAGE, Principles for Happiest Marriage”.  Ndani ya kitabu hiki utajifunza namna ipasayo ili kuwa na mahusiano ya ndoa imara kuanzia uchumba hadi malezi bora ya watoto kwa kadiri utakavyo barikiwa na Mungu. Kila mmoja anakihitaji kitabu hiki, siyo wana ndoa peke yao, hata vijana wanaotarajia kufunga ndoa miaka michache ijayo.

Kitabu cha pili kinaitwa, “EFFECTIVE TALKING WITH GOD, Becoming God’s Friend”.  Katika kitabu hiki utajifunza kukuza imani yako na uhusiano wako na Mungu, namna sahihi ya kujihudhurisha mbele za Mungu na kufikia viwango vya kuwa rafiki wa Mungu. 

Vitabu hivi bado havijawa tayari kwa sasa, vipo katika hatua ya “peer reviewing” ili kuhakiki ubora wake. Miezi michache ijayo, vitabu vyote vitakuwa vinapatikana sokoni na vitauzwa na wauzaji wa kimataifa kwa njia ya mtandao kama Amazon.com. Vitabu vyote vimeandikwa kwa lugha ya Kiingereza ili kuvipa wigo mkubwa zaidi wa wasomaji kwa Jina la Yesu Kristo. 

Usipange kuvikosa vitabu hivi, na Mungu atakubariki sana. Amina.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts