Saturday, August 25, 2012

SENSA


  Luka 2:1-5 “… Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbali na jamaa ya Daudi; ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa, naye ana mimba”.  
Ukisoma kwa makini katika mistari ya injili hiyo hapo juu kama ilivyoandikwa na Mwinjili Luka; neno linatuambia kuwa Yusufu alifunga safari yeye pamoja na Mariamu mkewe ambaye alikuwa mjamzito (mwenye ujauzito wa Bwana wetu Yesu Kristo) kutoka mji aliokuwa anaishi wa Nazareti ulioko Galilaya na kwenda katika mji wa Daudi yaani Bethlehemu ulioko Uyahudi. Kilichomfanya afanye safari ile ni amri iliyotolewa na Kaisari Augusto, iandikwe orodha ya majina ya watu wotewa ulimwengu (ambayo ilikuwa ni orodha ya kwanza kuandikwa hapo Kirenio).
  Hiyo ilikuwa ni sensa inayofanana na hii tunayoifanya wananchi wa Tanzania kwa mujibu wa katiba kila baada ya miaka kumi, ili kuijua idadi yetu na hivyo kuipa urahisi serikali yetu katika mipango yake ya maendeleo kwa sekta mbali mbali za kijamii kama afya, elimu, miundombinu n.k. Kuna baadhi ya wenzetu wamekuwa wakiihususha shughuli hii na ushirikina na wapo ambao wamekuwa wakiipinga kwa sababu zao binafsi aidha za kimaslahi au kisiasa. Kwa mkristo yoyote kukataa kuhesabiwa kwa kujishawishi yeye mwenyewe au kwa ushawishi wa mtu mwengine yoyote ni kwenda kinyume na neno la Mungu na hivyo ni kosa kama kuivunja amri yoyote ya Mungu, kama biblia inatuonesha Yusufu na mkewe Mariamu walihesabiwa na wewe hutaki kuhesabiwa ni kosa.

Sunday, August 19, 2012

MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE


  Kutoka 15:26 “…kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye.” Watu wengi wamekuwa wakihangaika kwenda huku na huko wakitafuta uponyaji wa magonjwa na madhaifu ya namna mbali mbali yanayowasumbua katika afya za miili yao, inawezekana ukawa wewe au ndugu yako wa karibu. Na mara nyingine utawakuta watu wa namna hii wamefikia hata hatua ya kwenda kwa waganga wa kienyeji. Ngoja nikufungue akili utambue kitu; ili mtu awe daktari ni lazima afundishwe na madaktari masomo yanayohusu udaktari, na ili mtu awe mganga wa kienyeji ni lazima afundishwe uganga wa kienyeji na mganga wa kienyeji. Na ukikuta mganga wa kienyeji anasema ngoja tuiulize mizimu ama kwa lugha nyingine wanawaita waungwana utambue moja kwa moja kuwa uganga wake una mahusiano na nguvu za giza (uchawi). Ni vema kutumia chakula; mboga za majani na matunda kwa kujenga na kulinda afya yako na hata kutibu baadhi ya magonjwa kama masomo yapatikanayo katika ukurasa wa dondoo za afya (Health Tips)  yanavyokuelekeza.
  Napenda nikwambie kama jinsi Mungu anvyosema, “Mimi ndimi Bwana nikuponyaye” anamaanisha anachokisema na kamwe Mungu hajawahi na hatawahi kusema uongo. Hebu tuangalie ahadi nyingine za neno la Mungu kuhusu kutuponya na magonjwa na madhaifu yanayotupata:-

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts