Saturday, August 25, 2012

SENSA


  Luka 2:1-5 “… Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbali na jamaa ya Daudi; ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa, naye ana mimba”.  
Ukisoma kwa makini katika mistari ya injili hiyo hapo juu kama ilivyoandikwa na Mwinjili Luka; neno linatuambia kuwa Yusufu alifunga safari yeye pamoja na Mariamu mkewe ambaye alikuwa mjamzito (mwenye ujauzito wa Bwana wetu Yesu Kristo) kutoka mji aliokuwa anaishi wa Nazareti ulioko Galilaya na kwenda katika mji wa Daudi yaani Bethlehemu ulioko Uyahudi. Kilichomfanya afanye safari ile ni amri iliyotolewa na Kaisari Augusto, iandikwe orodha ya majina ya watu wotewa ulimwengu (ambayo ilikuwa ni orodha ya kwanza kuandikwa hapo Kirenio).
  Hiyo ilikuwa ni sensa inayofanana na hii tunayoifanya wananchi wa Tanzania kwa mujibu wa katiba kila baada ya miaka kumi, ili kuijua idadi yetu na hivyo kuipa urahisi serikali yetu katika mipango yake ya maendeleo kwa sekta mbali mbali za kijamii kama afya, elimu, miundombinu n.k. Kuna baadhi ya wenzetu wamekuwa wakiihususha shughuli hii na ushirikina na wapo ambao wamekuwa wakiipinga kwa sababu zao binafsi aidha za kimaslahi au kisiasa. Kwa mkristo yoyote kukataa kuhesabiwa kwa kujishawishi yeye mwenyewe au kwa ushawishi wa mtu mwengine yoyote ni kwenda kinyume na neno la Mungu na hivyo ni kosa kama kuivunja amri yoyote ya Mungu, kama biblia inatuonesha Yusufu na mkewe Mariamu walihesabiwa na wewe hutaki kuhesabiwa ni kosa.

  Warumi 13:1-7 “kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwaS Mungu; na ile iliyopo imeamriwa na Mungu ….”.
Neno la Mungu halijachanganua ni mamalaka ya kidini au kiserikali, limesema mamlaka ambazo ni mamalaka ya uongozi wa dini na wa serikali. Kufanya kinyume na maagizo ya mamlaka hizo mbili ni kufanya kosa na neno la Mungu linatuambia mtu huyo anastahili hukumu. Kwetu wakristo hukumu ni mara mbili; hukumu ya kwanza ni kutoka serikalini na hukumu ya pili ni kutoka kwa Mungu mwenyewe kwa kutokulitii neno lake. Hivyo kwa kila mkristo anayemwamini Mungu na Yesu Kristo Bwana wetu na lazima ahesabiwe, achana na dhana na fikra potofu ulizo nazo au unazozisikia kutoka kwa watu wengine, itii serikali yako na ulitii neno la Mungu pia.
Mkristo unatakiwa uwe muhamasishaji wa kwanza wa jambo hili (sense); wahamasishe jamaa, marafiki na ndugu watoe ushirikiano wa dhati na unaotakiwa katika zoezi hili tangu kuanza kwake na hata kumalizika kwake.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts