Saturday, September 15, 2012

MAKUSUDI YA KUUMBWA MWANADAMU


   Baada ya Lucifer (ibilisi) kuasi, Mungu na Utatu wake Mtakatifu waliamua kumfanya/kumuumba mtu kwa mfano wao. Mtu ambaye walimuumba kwa mfano wao; ambaye ana roho, nafsi na mwili.
Mwanzo 1:26 “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu…”. Katika mstari huo wa kitabu kitakatifu cha Mungu, Biblia tunaona kuwa Mungu alikuwa akifanya makubaliano na mtu au watu zaidi ya mmoja juu ya kumuumba mtu au mwanadamu. Na aliokuwa akifanya nao maamuzi ya uumbaji wa mtu ni nafsi zake mbili, yaani Mungu mwana (Yesu Kristo) na Mungu Roho Mtakatifu. Mungu katika Utatu wake Mtakatifu ndiye aliye amua kumuumba mtu au mwanadamu kwa ajili ya utukufu wake, na mwanadamu huyu aliumbwa kwa makusudi maalumu ya Mungu mwenyewe.
Inaaminika kwamba Lucifer (ibilisi) alikuwa miongoni mwa malaika wakuu watatu wa Mungu, wengine wakiwa ni Malaika Gabrieli na Malaika Mikaeli amabaye ni malaika wa vita. Wakati ule Lucifer (ibilisi) alikuwa ni malaika mkuu wa sifa, ambaye alikuwa akimpa Mungu utukufu kwa jinsi ya maumbile yake.
Katika ufalme wa Mungu, muundo wa uongozi wa Mungu ulikuwa hivi; Utatu Mtakatifu wa Mungu ndiyo ulikuwa mkuu ukifuatiwa na Malaika hao Wakuu watatu (Lucifer, Gabriel na Michael) na hatimaye walifuatia malaika wengine.
Lakini Lucifer (ibilisi) alipokubali kumuasi Mungu ili akiinue kiti chake juu zaidi ya kiti cha enzi cha Mungu, akitaka kujipa nafasi ya Mungu ndipo aliponyang’anywa utukufu aliokuwa nao na kutupwa hadi kuzimu amabko anatawala jeshi la malaika wao waliokubali kuungana naye katika kumpindua Mungu. Malaika hao waovu ndiyo wajulikanao kama mapepo hivi leo kutoka ufalme wa giza ambao idadi yao ilikuwa ni theluthi ya malaika waliokuwepo Mbinguni wakati ule.
“Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, nitakiinua kiti change juu kuliko nyota za Mungu; name nitaketi juu ya mlima wa mkutano, katika pande za mwisho za kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu, nitafanana nay eye Aliye juu. Lakini utashushwa mpaka kuzimu, mpaka pande za mwisho za shimo” Isaya 14:13-15.
“Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama” Ezekieli 28:17
Mistari ya Biblia hiyo hapo juu unatuonesha jinsi Lucifer ajulikanae kama ibilisi au shetani baada ya kutupwa kuzimu jinsi alivyoasi na kutwa hadi kuzimu. Na kutupwa kwa ibilisi kuzimu haikuwa jambo rahisi, kwani kulitokea vita kati yake na wafuasi wake dhidi ya jeshi la Malaika wa Mungu wakiongozwa na Malaika wa vita Mikaeli.
“Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi.” Ufunuo 12:4(a). katika Biblia, kitabu hicho cha Ufunuo wa Yohana tunaoneshwa idadi ya malaika walioasi pamoja na ibilisi, ambao kwa lugha ya ufunuo wamefananishwa na nyota.
“Kulikuwa na vita mbinguni, Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana pamoja nao na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye ibilisi na shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi na malaika zake wakatupwa pamoja naye” Ufunuo 12:7-9.
Baada ya kutupwa hata kuzimu, shetani na malaika zake ambao kwa sasa ndiyo mapepo wakaamua kutengeneza ufalme wao ujulikanao kama ‘ufalme wa giza’ ambao unafanya kazi kinyume na “Ufalme wa Mungu”, ufalme huo wa giza ndiyo uafalme uletao mateso hapa duniani; magonjwa, vita na hali ngumu ya uchumi na mengine yafananayo na hayo. Ashukuriwe Mungu aliyetupa damu ya Mwana Kondoo (Yesu Kristo) ambayo kwa hiyo tunamshinda shetani na ufalme wake wa giza. Na ili kumshinda ni lazima kujikana, na kujikana kwenyewe ni kuamua kumpokea Yesu Kristo kuwa mwokozi wako na kuishi maisha ya utakatifu.
“Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao… Ufunuo 12:11”. Mstari huo wa kitabu kitakatifu, Biblia unatufundisha ni jinsi gani tunaweza kumshinda shetani na ufalme wake wa giza.
Baada ya shetani na ibilisi kutupwa kuzimu, ndipo Utatu Mtakatifu wa Mungu ulipoazimia kumuumba mwanadamu. Na ile nafasi aliyokuwa nayo sheteni katika uongozi wa Ufalme wa Mungu akakabidhiwa mwanadamu huyo. Yaani ngazi ya pili ya ukuu; baada ya Utatu Mtakatifu wa Mungu ndipo mwanadamu huyo anchukua nafasi akifuatiwa na malaika. Na ieleweke kwamba si kila mwanadamu anachukua nafasi hiyo, isipokuwa ni yule tu aliyekubari kuishi kwa kuyatimiza mapenzi ya Mungu. Ni mwanadamu au mtu yoyote aliye na Ufalme wa Mungu ndani yake. “Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, Ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza…., Ufalme wa Mungu umo ndani yenu. Luka 17:20-21”. Na hili ni moja ya majukumu au makusudi ya Mungu kumuumba mwanadamu, ili Ufalme wake uwakilishwe hapa duniani kama Mbinguni. Na mwanadamu aliyemkamilifu mbele za Mungu ndiye anayeuwakilisha Ufalme wa Mungu hapa duniani.
“Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii. Ufunuo 19:10”. Huyo aliyetaka kusujudu ni Yohana Mtakatifu, na aliyetaka kumsujudia ni malaika aliyekuwa akimuonesha maono ya Mbinguni. Malaika yule akamwambia ‘usifanye hivyo, mimi ni mjoli wako’, maana yake yeye (malaika) ni mdogo kwake. Na aliposema ‘na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu’, alimaanisha na kila mwanadamu aliyempokea Yesu Kristo kuwa mwokozi wake.
“Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake. Msifuni kwa matendo yake makuu; msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake. Msifuni kwa mvumo wa baragumu; msifuni kwa kinanda na kinubi; msifuni kwa matari na kucheza; msifuni kwa zeze na filimbi; msifuni kwa matoazi yaliayo; msifuni kwa matoazi yavumayo sana. Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.” Zaburi 150.
Hiyo ni sababu nyingine au makusudi ya Mungu kumuumba mwanadamu au kumfanya mtu kwa mfano wake, mwanadamu huyu ampe Mungu sifa anazo stahili kutoka na matendo yakemakuu yenye utukufu. Hivyo basi watu wote na tumwimbie Mungu nyimbo za sifa na kutamka sifa midomoni mwetu kwa ajili ya Mungu wetu.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts