Sunday, July 21, 2013

UNAWEZA KUWA UNATEMBEA CHINI YA LAANA PASIPO WEWE MWENYEWE KUJUA.



YESU KRISTO ASIFIWE!

Ashukuriwe Mungu aliyetupa kibali cha mimi na wewe msomaji wangu kukutana leo ikiwa ni kwa mara ya kwanza au kwa mara nyingine tena. Leo tuna somo lenye kichwa kisemacho “UNAWEZA KUWA UNATEMBEA CHINI YA LAANA PASIPO WEWE MWENYEWE KUJUA”, katika somo hili tutaangalia kwa undani mambo yafuatayo:-


  • Maana ya laana.

  • Laana inaletwa/sababishwa na nani?

  • Kwa nini ulaaniwe?

  • Je, unaweza kuwa umelaaniwa pasipo wewe kujua?

  • Ni vitu gani vinaweza kulaaniwa?

  • Kuvunja laana na mikosi, kuomba baraka za Mungu (Yehova).

Hili ni somo zuri sana ambalo ukilifuatilia kwa ukaribu zaidi na ukijenga imani kwa Mungu kuna vitu (laana), Mungu anakwenda kuzivunja, kuzifuta na kuziharibu (1 Yohana 3:8) na kuyabadilisha maisha yako kabisa. Unakwenda kuishi maisha ya baraka na ushindi, nakuhakikishia lazima utazishuhudia baraka za Mungu katika maisha yako baada ya kumaliza somo hili.

Maana ya laana.
Laana ni bahati mbaya au maneno mabaya ya maapizo yanayotamkwa kumuelekea mtu fulani yeye mwenyewe au kitu fulani kinachomuhusu, kwa mfano; kazi, shamba, watoto, masomo n.k kwa makusudi ya kumdhuru mtu huyo au kitu kinachomuhusu. Kwa kifupi laana ni kinyume cha baraka.

Laana inaweza ikasababishwa kwa makusudi maalumu (mfano: laana ambayo ni matokeo ya dhambi za wanadamu) au pasipo kujua (mfano: laana ya kujitamkia sisi wenyewe), kwa njia zote hizi mbili laana inafanya kazi iwe kwa makusudi au pasipo kujua.

Laana, ili itende kazi ni lazima iwe imeunganishwa na nguvu fulani zisizo za kawaida, nguvu za ziada “supernatural powers”,  nguvu hizo ni lazima ziwe zinazidi nguvu za mtu au kitu kinacholaaniwa. Nachomaanisha hapa ni kwamba, mdogo hawezi kumlaani mkubwa; shetani hawezi kumlaani Mungu, na mtu aliyesimama katika kweli na haki ya Mungu hawezi kulaaniwa na shetani kutokana na ile nguvu ya Mungu iliyomo ndani yake.

Kwa maana hiyo, kwa maneno yetu wenyewe au ya watu wa karibu nasi na matendo ya maisha yetu ndiyo sababu kubwa ya laana katika maisha yetu na vizazi vyetu vijavyo. Kwa sababu kila tunachokitamka na tunachokitenda kinafuatiliwa kutimilizwa na falme mbili tofauti; ufalme wa Mungu na ufalme wa shetani. Ni hakika na kweli, ufalme wa shetani hufuatilia hasa mambo ambayo ni hasi kuyatimiliza katika maisha yetu, kuwa mwangalifu sana.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts