Wednesday, August 21, 2013

HATUA NNE ZA KUPATA AMANI YA MOYO NA NAFSI (INNER PEACE).




Msongo wa mawazo na ukosefu wa amani moyoni na/au nafsini imekuwa ni tatizo linaloongezeka kwa kasi na kuwapata watu wengi sana. Na ubaya ama ugumu wa tatizo hili ni kwamba linagundulika baada ya matokeo ya ukosefu wa amani moyoni au nafsini na msongo wa mawazo.

Yaani ni hivi; watu wengi wasio na amani moyoni na nafsini huishi maisha ya kuigiza  na huwa vigumu sana kuwatambua watu hao, unaweza kumtambua mtu mwenye msongo wa mawazo kwa tabia yake ya kujitenga na kutoshirikiana na watu. Lakini unaweza usimtambue mtu asiye na amani moyoni au nafsini kwa sababu wengi wa watu hawa huvaa sura zenye tabasamu na furaha wawapo mbele za watu.

Ni watu wanaoyabeba maumivu yao wao wenyewe na kujaribu kutafuta suluhisho pasipo kuwashirikisha watu wengine. Na ndipo utakaposhangaa kuona mtu fulani amefanya jambo usilolitegemea alifanye, kwa mfano; kuua au kujiua wao wenyewe, kutukana matusi, au kufanya jambo la hatari ilihali anajua madhara yake pasipo kujihadhari.

Ndiyo, matokeo ya ukosefu wa amani moyoni au nafsini pamoja na msongo wa mawazo matokeo yake siku zote huwa ni hasara au maumivu kwa muhusika au watu wanao mzunguka. Wengi hutafuta njia za kutua mizigo iliyomo mioyoni na nafsini mwao kwa njia za mkato ambazo wengi hudhani kujiua au kuwaua wale wailowasababishia maumivu hayo ndiyo jibu sahihi.

Kuna nyakati ukosefu wa amani ya nafsi au moyo kunaambatana na chuki na visasi, yaani muhusika hubebea chuki na/au visasi dhidi ya mtu au watu waliomsababishia maumivu hayo. Kubeba chuki na visasi vya muda mrefu ndani ya mioyo na nafsi zilizokosa amani hupelekea matatizo ya kiafya kama shinikizo la damu (hypertension), mshituko (stroke), kupooza (paralysis) na hata kuzeeka mapema (early aging). Hii hutokea kwa watu ambao wana msongo wa mawazo, wamekosa amani moyoni na nafsini na huku wamebeba mizigo ya chuki na visasi dhidi ya watu wasioweza kuwalipia hicho kisasi.

Sisemi inatupasa kubeba chuki na visasi mioyoni na nafsini mwetu, hiki ni kitu kinachotupata nje ya uwezo wetu (involuntary action). Na kama jinsi tumekosa amani mioyoni na nafsini mwetu pasipo kupenda sisi wenyewe, ndivyo ilivyo ni vigumu kuitafuta amani ya nafsi na mioyo yetu sisi wenyewe pasipo msaada wowote.

Ni lazima utafute msaada, na msaada pekee na wa kuaminika ni Mungu (Yehova) peke yake. Ndiyo, kuna wanasaikolojia waliobobea ambao wanaweza wakakusaidia, lakini msaada wa Mungu kupitia Yesu Kristo ndiyo una uhakika wa asilimia mia moja (100%).

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts