Friday, November 9, 2012

MSAMAHA.


   Msamaha ni kufuta au kuachilia mzigo wa makosa unayotendewa na mtu pasipo kuhesabu ni mara ngapi mtu huyo amekukosea.
Isaya 43:25 “Mimi, naam, mimi ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe; wala sitazikumbuka dhambi zako”.
Hapo neno la Mungu linatufundisha kuwa; msamaha ni kuyafuta makosa (dhambi) na kutoyakumbuka tena.
Luka 6:37b “…achilieni, nanyi mtaachiliwa”.
Hapa tunaona kuwa maana nyingine ya msamaha ni kuachilia; mtu anaposhindwa kusamehe anabeba mzigo wa hasira ndani ya moyo wake, ambapo mzigo huu unaweza kumfanya mtu huyu akose raha, amani na hata furaha. Hapo Mungu anatuambia tuachilie na kutua mizigo iliyo ndani ya mioyo yetu.
AINA ZA MSAMAHA.
Kuna aina mbili za kusamehe, aina hizi ni;
(a). Msamaha wa kidunia.
Huu ni msamaha wa kusamehe na kutosahau. Msamaha huu hautokani na Mungu, na haukubaliki mbele za Mungu.
Ni msamaha wa kinafiki, mtu anakwambia amekusamehe lakini ndani ya moyo wake ana uchungu nawe. Msamaha huu unahesabu makosa, na wengu wameumia kwa sababu ya kusamehe kwa kutumia msamaha wa aina hii. Unapomwambia mtu nimekusamehe na kumbe bado una uchungu naye, yeye anapata amani na furaha lakini wewe unajawa na uchungu na hasira inayokufanya uumie moyo.
Wengi wetu tumekuwa na msamaha wa aina hii, Mungu atusaidie tuwe na msamaha wa Kimungu kwani msamaha huu una raha na faida. Kuna watu wamekonda na hawana raha siyo kwa sababu ya maisha magumu, bali ni kwa sababu wanavinyongo na mizigo mizito ndani ya mioyo yao.
(b). Msamaha wa Kimungu.
   Huu ni msamaha wa kusamehe na kusahau kabisa. Msamaha huu ni wa Mungu na unatokana na Mungu mwenyewe, kwani Mungu anasema yeye anatusamehe na kusahau kabisa makosa yetu (Isaya 43:25). Nasi kama watoto wa Mungu tunapaswa kuwa na tabia ya Mungu katika kusamehe, tunapaswa tusamehe na kusahau yote tunayokosewa na wenzetu.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts