Sunday, November 25, 2012

FANYA AGANO NA MUNGU KUPITIA SADAKA.

   Kutoa sadaka kama mazoea au desturi ni kupoteza fedha au mali yako pasipo na manufaa yoyote. Wapo wakristo ambao wamelelewa katika familia za dini na kukua wakijua ni lazima kwenda na sadaka ibadani lakini hawajui umuhimu na matunda wanayoweza kuyapata kwa kutoa sadaka. Wakristo wa namna hii ni kama watoto ambao wanapewa sadaka na wazazi wao, wakitoa au wasipotoa sadaka hiyo hawaoni mapungufu yoyote, zaidi ni faida kwao kwani watakula barafu.

   Na wapo wakristo wanaotoa sadaka kama ajali, wao huamua ni sadaka ya aina au kiasi gani watatoa muda mfupi baada ya kujianda kwenda ibadani au hata wakiwa njiani kuelekea ibadani. Wanatoa sadaka za kushtukiza, sadaka isiyo na maandalio yoyote.

   Sadaka inapaswa kuandaliwa, hata siku moja kabla ya kutolewa. Katika agano la kale utaona kuna siku zinapita tangu Mungu aombe kutolewa kwa sadaka na siku ya kuitoa hiyo sadaka, aliyeambiwa atoe sadaka anafanya maandalizi ya kuchagua sadaka nzuri ya kupendeza itakayopata kibali machoni pa Mungu.

   Sadaka utakayoitoa madhabahuni pa Mungu lazima uitamkie jambo. Kabla sijatoa sadaka yangu huwa namwambia Mungu hivi; “maadam, sadaka/dhabihu hii itafanya kazi shambani mwako ee Mungu wangu, fanya jambo (ninalitaja) katika maisha yangu”.
   Sadaka au dhabihu ni sawa na mbegu, ukipanda mbegu unategemea uzune kulingana na mbegu uliyoipanda. Sadaka au dhabihu ni mbegu ya kuvunia baraka zote za kiroho na kimwili, afya na uzima.

   Zaburi 50:5 “Nikusanyieni wacha Mungu wangu, Waliofanya agano nami kwa dhabihu (sadaka).
Agano ni makubaliano yasiyovunjika, kufanya agano na Mungu ni kujithibitishia makubaliano yako na Mungu kuwa yatatimia. Sasa unaweza ukafanya agano na Mungu kwa kutumia dhabihu au sadaka unayoitoa katika ibada zako, sadaka iliyoandaliwa na siyo sadaka ya kutolewa kama bahati mbaya. Agano hilo utalifanya pale utakapo itamkia neno sadaka unayoipeleka madhabahuni pa Mungu wako, ukitoa sadaka ambayo hukuitamkia neno utakuwa unatoa sadaka kama mtoto asiyejua nini maana ya sadaka na inatolewa kwa sababu gani.

Featured Post

HAIJALISHI TUNAKOSEA MARA NGAPI? MUNGU NI MUAMINIFU KILA WAKATI

Nakusalimu kupitia Jina kuu lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu. Mungu wetu ni muaminifu, hajawahi kuse...

Popular Posts